Zaburi 121:1 Nitayainua macho yangu nitazame milima, Msaada wangu utatoka wapi? 121:2 Msaada wangu u katika BWANA, Aliyezifanya mbingu na nchi. 121:3 Hatauacha mguu wako usogezwe, Akulindaye hataki usingizi. 121:4 Tazama, hatasinzia wala hatalala usingizi mlinzi wa Israeli. 121:5 BWANA ndiye mlinzi wako, Bwana ni uvuli mkono wako wa kuume. 121:6 Jua halitakupiga mchana, Wala mwezi usiku. 121:7 BWANA atakulinda na mabaya yote, Atakulinda nafsi yako. 121:8 BWANA atakulinda kutoka kwako na kuingia kwako tangu wakati huu mbele, na hata milele.